Serikali yataka rudisho la uwekezaji lifikie zaidi ya asilimia 10

Serikali yataka rudisho la uwekezaji lifikie zaidi ya asilimia 10

Serikali inataka rudisho la uwekezaji ‘return on investment’ katika kampuni ambazo serikali inaumiliki wa hisa chache kuongezeka kutoka asilimia saba ya sasa hadi kufikia zaidi ya asilimia 10  katika mwaka ujao wa fedha

Dhamira hiyo ilielezwa  Machi 28, 2025, na Katibu Mkuu Kiongozi  Dkt. Moses Kusiluka wilayani Kibaha, mkoani Pwani, wakati wa kufunga mkutano wa siku tatu wa wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo serikali inaumiliki wa hisa chache. 

“Niwape changamoto ya kukuza rudisho la uwekezaji kutoka asilimia saba ya sasa kwenda zaidi ya asilimia 10 kwa mwaka ili kufikia azma  hii mnapaswa kuongeza ufanisi wa utendaji," alisema.

alisema Ofisi ya Msajili wa Hazina inasimamia jumla ya taasisi 308 ambapo kati ya hizo 56 ni zile ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache, jumla ya uwekezaji wa Shlilingi  trilioni 86.3, umefanywa katika taasisi hizo, huku kati ya kiasi hicho Shilingi  trilioni 2.9 trilioni zikiwekezwa kwenye kampuni ambazo serikali ina umiliki wa hisa chache na Shilingi trilioni 83.4 ikienda kwa taasisi ambazo serikali ina umiliki wa asilimia 100.   

Aidha, Balozi Kusiluka aliwapa changamoto wakurugenzi wa bodi za  kampuni ambazo ina hisa chache kuongeza ufanisi gawio kwa serikali.

 

Related Articles

Visitor Counter

000347
Today: 2
Yesterday: 2
This Week: 4
Last Week: 32
This Month: 2

Opening Hours

  • Monday: 8.30am–6.30pm
  • Tuesday: 10.00am–8.00pm
  • Wednesday: 8.30am–6.30pm
  • Thursday: 8.30am–7.00pm
  • Friday: 8.30am–3.00pm
  • Saturday: 8.30am–2.00pm
  • Sunday: 8.30am–2.00pm

Contact Us

Kanani A Road, Mumasama Street,

P.O.BOX, 137

Ngara, Tanzania

Mobile:  +255 744 172 741

Email: info@ishizwemedia.co.tz